MVAE KRISTO

*Somo:- MVAE KRISTO ILI UISHI*

*Prophet Jacob Opull Zacharia*
*PVIC KWIMBA – MWANZA*
+255(0)743765475
jacobopull@gmail.com
pvictz19@gmail.com

Bwana Yesu asifiwe wapendwa katika Bwana,
Nawasalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo.

Napenda nisime nawe kidogo juu somo hilk *Mvae Yesu ili uishi*

Kuvaa kitu ni kufunika mwili au sehemu ya mwili kwa kitu hicho, mfano onapo vaa nguo unafunika mwili ili usiwe uchi, unapo vaa soksi unafunika mkuu usiwe uchi.

Katika maisha yetu ya Kiroho vilevile kuna wakati tunakuwa uchi na kujawa na aibu ya kiroho inayopelekea kutokuwa na ujasiri hata wa kusimama mbele ya watu.

Uchi wa kiroho husababishwa na kukosekana kwa uwepo wa Mungu, yaani kutofunikwa na Roho mtakatifu.

Roho mtakatifu hutupa ujasiri wa kunena neno la Mungu kwa ujasiri, na ili tuwe na Roho mtakatifu kazima kwanza tukubali kumookea Yesu awe Bwana na mwokozi wa maisha yetu yaani *Tumvae Kristo*

*WAGAKATIA 3:26-29*
*26Kwa kuwa ninyi nyote mmkuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu . 27 Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo *mmemvaa Kristo.* 28 Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume waka mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu. 29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.

Katika mstari wa 27 Biblia inasema kuwa tuliobatizwa katika Kristo tumemvaa Kriso. Kama tumemvaa kristo basi Kristo amekuwa kinga yetu
Kristo amekuwa mtetezi wetu
Kama tumemvaa Kristo, Kristo amekuwa ngao yetu
Kama tumemvaa Kristo basi kristo amefanyika moonyaji wetu.

Maisha Yetu yanamtegemea Kristo kana vile mwili wako unavyoutegemea nguo uliyo vaa ili uoate joto na uukinge na maradhi, ndivyo maisha yetu ya Kiroho yanavyo muhitaji Yesu ili tupate joto la kiroho,
Ilitupate uzima wa milele ni lazima tumvae Kristo kwa kuvatizwa na Roho mtakatifu.

*WARUMI 13:12*
*Usiku umeendlea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza na kuzivaa silaha za nuru.*

Biblia inatuambia kwamba tuyavue matendo ta giza na kuvaa silaha za nuru.
Ili tuwe na silaha za nuru lazima kwanza tumpokee Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yetu na kufanya bidii kuishi kuishi katika utakatifu.

Utakatifu huo unapatikana tu kwa kumvaa Kristo.

Kristo alijitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili tukimuamini, tutafanyika kuwa watoto wa Mungu na tunakuwa na uzima wa milele *Yohana 3:16*

*Warumi:13.14*
*Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake.*

Ili uishinde tamaa ta Mwili na vishawishi vyote vya hapa duniani na kuurithi uzima wa milele ni lazima umvae Kristo Yesu ili afunike maisha yako.

Ukimvaa Kristo utapata nguvu ya kusimama na kumshinda adui. Haijalishi vita vya aina gani vitainuka juu yako,
Watakaporusha mishale yao hayatakupata kwa sababu mishale yao itafika kwa Yekwanza na hivyo havitaweza kukudhuru.

Ili adui akushinde lazima kwanza amshinde Yesu uliyemvaa.

Haleluya
Yesu ni yote katika yote.
Yeye ni mtetezi, ni mfariji ni ngome imara, yeye ni adui wa adui zetu, yeye ni mtesi wa watesi wetu, yeye ni ushindi wetu.

Mpoke Bwana Yesu leo, mvae awe baraka na ushindi kwenye maisha yako, nawe utarithi uzima wa milele.

Barikiwa sana
Shalom.